Wimbi La Siasa

Mwaka mmoja wa mapigano nchini Sudan kati ya jeshi la serikali na RSF

Informações:

Sinopsis

Wiki hii, ilikuwa ni mwaka mmoja wa vita nchini Sudan, kati ya jeshi la taifa chini ya Jenerali  Abdel Fattah al-Burhan na wanamgambo wa RSF wanaongozwa na Jenerali Mohammed Hamdan Dagalo. Mwaka mmoja baadaye, vita vimeendelea na kusababisha vifo vya maelfu ya watu, huku wengine Milioni 8.5 wakiyakimbia makaazi yao wakiwemo Milioni 1.8 waliokwenda kutafuta hifadhi katika nchi jirani kama Chad.