Gurudumu La Uchumi

Informações:

Sinopsis

Fahamu masuala kadha wa kadha kuhusu uchumi kama vile, namna ya kupambana na umaskini, mfumuko wa bei, kushamiri kwa matumizi ya dola na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia kwa nchi za Afrika. Mada hizi zinafanyiwa utafiti wa kina na zinazungumzwa kwa lugha rahisi inayoeleweka ili kukufanya uelewe na usichoke kusikiliza .

Episodios

  • Je Afrika inawezaje kutumia raslimali watu kwa maendeleo ya uchumi?

    02/08/2023 Duración: 10min

    Takwimu zinaonyesha kuwa rasilimali watu katika nchi za kusini mwa jangwa la Sahara, ilikuwa ndogo mno ikilinganishwa na mataifa mengine ya dunia, ambapo Uviko 19 na vita vya Urusi nchini Ukraine vilichangia.  Wiki hii Emmanuel Makundi anaangazia wito wa wakuu wa nchi za ukanda ili kuangalia namna bora zaidi ya kutumia nguvu kazi iliyoko barani Afrika kwa maendeleo.

  • DRC: Kushuka kwa thamani ya fedha na changamoto la wakimbizi wa ndani

    26/07/2023 Duración: 09min

    Wimbi la wakimbizi wa ndani pamoja nakushuka kwa thamani ya pesa za kongo dhidi ya dola za Marekani  kumesababisha kupanda kwa gharama za maisha katika miji kadhaa nchini jamuhuri yakidemokrasia ya Kongo. Makal aya Gurudumu la uchumi juma hili inaangazia kwa kina hali hii na mtayarishaji Emmanuel Makundi, ameshirikiana na mwandishi wa Goma Benjamini Kasembe pamoja na kuzungumza na mtaalamu wa uchumi kutoka Bukavu Bengeya Machozi.

  • Ujuzi kwa vijana na teknolojia

    12/07/2023 Duración: 10min

    Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, inaangazia siku ya "ujuzi kwa vijana duniani' inayoadhimishwa kila tarehe 15 ya mwezi Julai kila mwaka, lengo ni kuwawezesha walimu, wakufunzi na vijana kutumia ujuzi wao kwa maendeleo.Leo mtayarishaji amezungumza na Tukupala Mwalyolo, msichana anayeunda ndege zisizo na rubani 'drone', pamoja na Emmanuel Cosmas Msoka, kijana mbunifu wote wakitumia teknolojia kutafuta suluhu na wako Tanzania.

  • Faida ya mfumo wa malipo ya pamoja barani Afrika

    31/05/2023 Duración: 09min

    Mwezi Januari mwaka 2022, benki kuu pamoja na wakuu wa nchi za umoja wa Afrika, waliunga mkono mchakato ulioanzishwa na benki ya Afrexim, ambayo ilitengeneza mfumo wa malipo uliolenga kurahisisha ufanyaji wa malipo na manunuzi kati ya nchi na nchi, mtu na mtu na biashara kwa biashara barani Afrika. Mfumo huu unafahamika kama Pan-African payments and Settlement System PAPSS, kwa kiasi kikubwa unapunguza changamoto ya ufanyaji malipo kwa kutumia fedha za kigeni kama Dola, ambapo kupitia mfumo huu nchi, biashara au watu wanaweza kubadilishana huduma kwa kutumia fedha ya nchi husika.Lakini je, ni kwanini bado mfumo huu hauonekani kutoa jibu kwa tatizo lililoko hasa linapokuja suala la malipo au ununuzi wa biadhaa ambapo nchi zinalazimika kutumia dola ? Mbali na hili tutaangazia pia ikiwa uongezaji wa tozo na kodi ndio suluhu kwa nchi nchi za Afrika kukabikliana na changamloto za kifedha na kiuchumi.Makala  ya Gurudumu la uchumi juma hili, inaenda kuangazia masuala haya kwa kina.

página 2 de 2